Proverbs 8:1-6
Wito Wa Hekima
1 aJe, hekima haitani?
Je, ufahamu hapazi sauti?
2 Juu ya miinuko karibu na njia,
penye njia panda, ndipo asimamapo;
3 bkando ya malango yaelekeayo mjini,
kwenye maingilio, hulia kwa sauti kubwa, akisema:
4 c“Ni ninyi wanaume, ninaowaita;
ninapaza sauti yangu kwa wanadamu wote.
5 dNinyi ambao ni wajinga, pateni akili;
ninyi mlio wapumbavu, pateni ufahamu.
6 eSikilizeni, kwa maana nina mambo muhimu ya kusema;
ninafungua midomo yangu kusema lililo sawa.
Copyright information for
SwhKC